Wakili
wa Lady Jaydee, Mabere Marando (kulia) akimueleza jambo wakili wa
viongozi wa Clouds Media Group, Ruge na Kusaga, Willy Lusajo. Katikati
ni mume wa Anaconda, Gadna G. Habash.
Gadna akiondoka eneo la mahakama hiyo baada ya kesi kuahirishwa.
Gadna na Anaconda wakiwa ndani ya gari lao muda mfupi kabla ya kuondoka mahakamani.
KESI inayomkabili mwanamuziki wa kizazi
kipya nchini, Judith Wambura ‘Lady Jaydee’ a.k.a Anaconda ya kuwakashifu
baadhi ya viongozi wa kampuni ya Clouds Media Group, leo imekwama tena
kusikilizwa baada ya hakimu aliyeshikilia kesi hiyo katika Mahakama ya
Wilaya ya Kinondoni, Athuman Nyamlani kupatwa na hudhuru. Kesi hiyo
imepangwa kusikilizwa tena Agosti 6 mwaka huu mahakamani hapo.
Yafuatayo ni baadhi ya matukio yaliyojiri eneo la mahakama hiyo.
Yafuatayo ni baadhi ya matukio yaliyojiri eneo la mahakama hiyo.
( GPL)