
“Uongozi wa Hospitali unaomba radhi kwa usumbufu waliopata wagonjwa na wananchi waliofika hospitalini hapo kwani tangazo lilitolewa kimakosa na Katibu kwani lilikuwa likiwahusu watumishi pekee na si wananchi,” alisema Dk Mpuya.
Kwa mujibu wa tangazo hilo, Hospitali ya Mkoa wa Dodoma iliweka masharti ya uvaaji ambapo mavazi yaliyopigwa marufuku ni sketi fupi, fulana zisizo na mikono nguo za kubana pamoja na Jeans.
Juzi kulitokea kutoelewana kati ya walinzi na watu waliokuwa wakitaka kuingia hospitalini hapo na kuzuiwa kutokana na aina ya mavazi waliyokuwa wamevaa.