Akizungumza na Risasi Jumamosi, Chuchu alibainisha kuwa ni kipindi kifupi sana alichoishi na mumewe ambaye alikuwa mtangazaji wa Televisheni ya Channel Ten, Frank Mtao, ambaye sasa yupo Sidney, Australia kikazi.
“Unajua mimi nimeshazoea kabisa maisha ya ubachela na hata kuna wakati najisahau kama niliolewa kwa maana nimeshakaa peke yangu muda mrefu sana lakini nashukuru Mungu nina marafiki wengi wanaonipa kampani hivyo upweke unaondoka,” alisema Chuchu.