Hivi ndivyo Wekundu wa Msimbazi Simba SC walivyobondwa 3-1 na Timu ya Jeshi la Oman.


Samba SC

 v/s

Jeshi la Oman

Mabingwa wa soka Tanzania, Simba SC  walifungwa mabao 3-1 katika mechi ya kirafiki dhidi ya timu ya taifa ya Jeshi la Oman.


 
Mechi hiyo  ilichezwa Ijumaa jioni kwenye uwanja wa Qaboos complex jijini Muscat.
Bao la simba lilifungwa katika kipindi cha pili na Haruna Moshi 'boban'.

Mwenyekiti wa Simba Ismail Aden Rage

 akiwa na wenyeji wake huko Oman

wakiangalia Simba ikisurubiwa

 na wanajeshi.
Mwenyekiti wake Ismail Aden Rage alikuwa jukwaani pamoja na viongozi wengine wa Simba, Rahma Al Kharusi na Musleh Rawahi pamoja na kocha Talib Hilal wakiishuhudia simba ikizama mbele ya wanajeshi hao ambao kikosi chao kina wachezaji tisa wanaocheza timu ya taifa ya Oman.

Boban na wenzake wakishangilia goli 
lao 1-3 katika mchezo huo.


Wachezaji Kaseja, Mwinyi Kazimoto, Mrisho Ngassa, Sunzu wakiwa benchi huku wakizungumza na mfadhili wa safari yao Bi.Rahma na mwenyekiti wao Aden Rage.

Simba SC  1 - 3 Timu la Jeshi la Oman.
back to top