Suarez aadhibiwa na kocha wake.

Luis Suarez akiwa mwenyewe kwenye uwanja wa mazoezi wa Liverpool huko Melwood.

Luis Suarez akiwa mwenyewe kwenye uwanja wa mazoezi wa Liverpool huko Melwood.
Kocha wa klabu ya Liverpool Brendan Rogers amemuamuru mshambuliaji wa klabu hiyo Luis Suarez kufanya mazoezi mwenyewe ikiwa ni hatua ya kinidhamu kwa mshambuliaji huyo kwa kitendo ambacho kocha wake alikiita kuikosea Liverpool heshima .

 Rogers amechukua hatua hiyo baada ya Suarez kuzungumza na vyombo vya habari ambapo alisema kuwa klabu yake ilimuahidi kumuuza endapo ingeshindwa kufuzu michuano ya ligi ya mabingwa ahadi ambayo Liverpool wanaonekana kuivunja .
Sakata linalohusu mustakabali wa mshambuliaji huyo ndani ya Liverpool linazidi kuwa gumu kadri siku zinavyoenda na kwa sasa wakala wa mshambuliaji huyo amekuwa akihangaika kulazimisha kuondoka kwake huku klabu ya Arsenal ikiwa inataka kumsajili.
Kocha wa Liverpool Brendan Rogers amemuadhibu Suarez kwa kumtaka afanye mazoezi mwenyewe.

Kocha wa Liverpool Brendan Rogers amemuadhibu Suarez kwa kumtaka afanye mazoezi mwenyewe.
Suarez alizungumza na vyombo vya habari siku ya jumatatu ambapo alifunguka na kusema kuwa Liverpool iliahidi kumuuza kama ingeshindwa kufuzu michuano ya ligi ya mabingwa barani ulaya .
Hata hivyo imegundulika kuwa kipengele ambacho kipo kwenye mkataba wa Suare z ambacho wakala wa mchezaji huyo na mchezaji mwenyewe walidhani kinatoa ruhusa ya kuuzwa kwa klabu yoyote ambayo itafikia bei ya paundi milioni 40 hakiko kama walivyodhani na badala yake kinasema kuwa endapo itajitokeza klabu yenye nia ya kumnunua Suarez klabu itamtaarifu kuwa kuna klabu inamtaka pasipo kulazimika kumuuza .
Wakala wa Luis Suarez ambaye ni mdogo wa kocha wa Barcelona Pere Guardiola amekuwa akihangaika na wanasheria toka Hispania kubadilisha kipengele hicho ili kutoa fursa kwa Suarez kuuzwa .
Kesi hiyo huenda ikahamia kwa viongozi wa ligi kuu ya England na umoja wa wachezaji PFA ambao wamekuwa wakifuatilia kesi hiyo kwa ukaribu.
back to top