matukio ya ubakaji kwa wanafunzi: Shuleni, barabarani kote sio salama

Wanafunzi wa shule ya msingi Hekima waliohudhuria tamasha la kukataa ubakaji lililofanyika hivi karibuni 
Ripoti ya hivi karibuni inasema vitendo vya ubakaji na ulawiti wanavyofanyiwa wanafunzi vimeshika kasi maeneo mbalimbali nchini, hususan visiwa vya Zanzibar na jiji la Dar es Salaam

Changamoto mbalimbali zinawakabili wanafunzi nchini, hasa wanaosoma katika madaraja ya chini ya elimu.
Miongoni mwa changamoto hizo ni pamoja na kushamiri kwa vitendo vya ubakaji na ulawiti, wanavyofanyiwa watoto chini ya umri wa miaka 18.
Ripoti ya utafiti wa hivi karibuni iliyotolewa na Chama cha Wanahabari Wanawake Tanzania (Tamwa), inasema ubakaji umeshika kasi maeneo mbalimbali nchini, hususan visiwa vya Zanzibar na jiji la Dar es Salaam.
Kwa mujibu wa utafiti huo uliohusu kuangalia vitendo vya ukatili na unyanyasaji wa kijinsia, sababu kuu zinazochangia kuongezeka kwa vitendo hivyo ni umaskini na tamaa iliyopitiliza kwa baadhi ya wanaume.
Mkurugenzi wa Tamwa Valerie Msoka, anasema ukatili kupitia ubakaji umekithiri katika maeneo mengi nchini, na vitendo hivyo hutokea zaidi wanafunzi wanapokwenda shule na hata ndani ya familia.
Wakati ndani ya familia vitendo hivyo vinatajwa kufanywa na wanandugu, wanafunzi wengi hawana amani hasa wanapokwenda ama kurudi shuleni kwa kutumia barabara ambazo ni hatarishi. Hawa ni wale wanafunzi wanaoishi mbali na maeneo ya shule.
“Katika wilaya 10 na vijiji 60 vya Tanzania bara na Zanzibar vilivyofanyiwa utafiti, inaonyesha kuwa ukatili wa kubakwa na ulawiti kwa wanafunzi ni mkubwa kiasi cha watoto kukosa fursa yao ya msingi ya kupata elimu,” anaeleza.
Akirejea baadhi ya tafiti zilizokwishafanywa siku za nyuma, anasema matukio ya ukatili huo yanasababishwa na mambo kadhaa, yakiwemo ulevi, imani za kishirikina, umaskini katika familia na tamaa iliyopitiliza kwa baadhi ya wanaume.
Hata hivyo, anasema juhudi za kupambana na hali hii zinakosa nguvu, kwani hata matukio yanapotokea na kuripotiwa katika vyombo vya dola, watuhumiwa hawafikishwi mahakamani.
Aidha, anaeleza kuwa kwa wale wanaofikishwa mahakamani, huachiwa katika mazingira ya kutatanisha yanayochochewa na rushwa kwa kisingizio cha kukosekana ushahidi.
“Tatizo lingine ni baadhi ya wananchi kuamua kusuluhisha tatizo la ubakaji katika ngazi ya familia, kwa madai ya kuona aibu katika jamii, kutojua haki zao na uelewa mdogo wa sheria zinazoshughulikia makosa ya ubakaji,” anaongeza kusema.
Ukubwa wa tatizo
back to top