
Taarifa toka nchini Ujerumani ambazo zimeripotiwa kwenye gazeti moja la jioni linalofahamika kwa jina la Welte zinasema kuwa kiungo wa kimataifa wa Brazil Luiz Gustavo amekubali kujiunga na klabu ya Bundesliga ya Wolfsburg .
Awali kulikuwa na taarifa za kuthibitika kuwa kiungo huyo alikuwa karibu kujiunga na Arsenal baada ya klabu yake ya Bayern Munich kuikubali ofa ya Arsenal ya Euro Milioni 19 kwa ajili ya kumnunua .
Wolfsburg ndio ilikuwa timu ya kwanza kufanya jitihada za kumsajili Luiz Gustavo baada ya mchezaji huyo kuwekwa kwenye Orodha ya wachezaji watakaouzwa kwa kuwa hayupo kwenye mipango ya kocha Pep Guardiola .
