Hivi ndivyo Chameleone aliweka historia kwenye Badilisha Live show April 26Weekend
hii star wa 'Valu Valu' Jose Chameleone lutoka nchini Uganda ameongeza kitu
kikubwa katika historia ya career yake baada ya kufanya onesho lenye
mafanikio makubwa Ijumaa ya April 26, 2013 katika viwanja vya Kyadondo
Rugby club Kampala Ug. Show hiyo iliyohudhuriwa na mashabiki wapatao 20,000 ilionekana kuwa na
maandalizi makubwa sana kwa mujibu wa watu waliohudhuria. Baadhi ya wasanii
waliopewa mualiko ni pamoja na Prof Jay kutoka Tanzania, Red San kutoka
Kenya na wengine.
Josee Chameleon akiwa na mwanae kushoto wote wakiwa jukwaani wamekula pozi.
"Daniella" mke wa Chameleon (kushoto) akiwa na wenzake wakati wa uzinduzi huo.
Redsan katikati akiwa na Prof Jay wakimtazama Jose Chamelion akifanya yake jukwaani.