Mabingwa watetezi wa FA Cup Chelsea waivuruga Southampton.

  

 

Demba Ba

Mabingwa watetezi Chelsea wameanza vyema utetezi wao kwa kuivurumisha Southampton Bao 5-1 kwenye Mechi ya Raundi ya 3 ya FA Cup iliyochezwa nyumbani kwa Southampton.


Aidha raund ya 3 ya FA CUP Januari 5,2013 imeshuhudia Timu za Ligi Kuu Uingereza Aston Villa, Reading, Manchester  City, Norwich, Chelsea na Spurs zikisonga kuingia Raundi ya 4 huku Sunderland, Stoke, Fulham, QPR, West Brom na Wigan zikiambulia sare na itabidi kucheza Mechi za marudiano lakini Newcastle walipata aibu kwa kubwagwa nje walipofungwa 2-0 na Brighton inayocheza Daraja la chini.
back to top