SANDRA: WASANII TUMRUDIE MUNGU

 
Msanii wa filamu Bongo, Salma Salmin ‘Sandra’ akilia kwa huzuni baada ya kifo cha Adam Kuambiana.

KUFUATIA kifo cha msanii mkongwe wa filamu Bongo, Adam Kuambiana, msanii mwenzake, Salma Salmin ‘Sandra’ amewataka wasanii kubadili mfumo wa maisha na kumrudia Mungu.

 
Baadhi ya wasanii na jamaa wa karibu wa marehemu Adam Kuambiana wakiuchukua mwili.
Akizungumza na paparazi wetu katika Hospitali ya Mama Ngoma, Mwenge jijini Dar ulipokuwa mwili wa Kuambiana kabla haujahamishiwa Muhimbili, Sandra alisema ameumizwa sana na kifo cha msanii huyo kwani kimekuwa cha ghafla sana hivyo ni fundisho kwao wasanii kwamba wanatakiwa kumrudia Mungu na kuwa watu wa sala muda wote kwani kifo kipo na hakina muda maalum.
Aliongeza kuwa haifai wasanii kuwa na mabifu ya kijinga badala yake wapendane kwani hawajui kifo kitawakuta wakiwa wanafanya nini.
back to top