Alichosema Eto’o kuhusu Chelsea, cheki hili box la mgawanyo wa mshahara wake na wa wachezaji wa dunia.

Samuel Eto'o huenda akaungana na Mourinho kwa mara nyingine.
Samuel Eto’o huenda akaungana na Mourinho kwa mara nyingine.
Mshambuliaji wa timu ya taifa ya Cameroon Samuel Eto’o huenda akaungana na kocha wake wa zamani Mreno Jose Mourinho baada ya kuweka wazi utayari wake wa kujiunga na Chelsea endapo nafasi hiyo itajitokeza.

Eto’o amewekwa kwenye orodha ya wachezaji wanaotarajia kuuzwa na klabu ya Anzhi Makhachkhala ya Urusi baada ya bosi wa klabu hiyo kubadili sera ya usajili toka kwenye kusajili wachezaji nyota wenye majina makubwa na wanaolipwa mishahara minono na kuamua kujenga timu yenye wachezaji wa bajeti ya chini.
Kwa muda wa miaka miwili Eto’o amekuwa mchezaji anayelipwa fedha nyingi kuliko wote duniani baada ya kukubali kujiunga na Anzhi ya Urusi akitokea Inter Milan ambako alicheza kwa miaka miwili baada ya kuondoka Barcelona.
Kundi la wachezaji raia wa Urusi wakiongozwa na nahodha wa timu ya taifa hilo Igor Denisov walianzisha mgomo baridi ndani ya kambi ya Anzhi Makhachkhala dhidi ya wachezaji wageni wanaolipwa fedha nyingi kama Eto’o hali ambayo imesababisha mwenyekiti wa timu hiyo kubadili sera ya usajili na uendeshaji wa timu hiyo.
Sambamba na Eto’o, staa kama Lassana Diarra, Lacina Traore, Christopher Sambana wengineo wanatarajiwa kuuzwa kwa timu zinazowahitaji.
Kwenye sentensi nyingine ni kwamba siku kadhaa zilizopita Anzhi ilitangaza kumfukuza kazi kocha wake Rene Meulenstein ambaye alikuwa amekaa na timu hiyo kwa mwezi mmoja pekee akiwa amekuwa kocha mkuu kwa muda wa siku kumi na sita baada ya kushika nafasi hiyo kufuatia kujiuzulu kwa kocha Guus Hiddink.
Mgawanyo wa mshahara anaopata Eto'o ndani ya klabu ya Anzhi Makhachkhala.
Mgawanyo wa mshahara anaopata Eto’o ndani ya klabu ya Anzhi Makhachkhala.
Eto'o anaongoza kwa kulipwa mshahara mkubwa kuliko wachezaji wote duniani.
Eto’o anaongoza kwa kulipwa mshahara mkubwa kuliko wachezaji wote duniani.
Eto’o mwenyewe ameonekana kuvutiwa na uwezekano wa kuungana na kocha wake wa zamani ambaye walifanya kazi kwa mafanikio ndani ya Inter Milan ambapo klabu hiyo ilitwaa mataji matano katika kipindi cha misimu miwili.
Chelsea itamsajili Eto’o endapo itashindwa kumsajili mshambuliaji wa Manchester United Wayne Rooney ambaye Mourinho amemtangaza kuwa chaguo lake namba moja kwenye usajili wake.
back to top