AUNT LULU AAMUA KUACHANA NA MASHOGA
MWIGIZAJI wa sinema za Kibongo, Lulu
Semagongo ‘Aunty Lulu’ amepigwa ‘stop’ kutembea na marafiki wanaodaiwa
kuwa ni wanaume wenye vitendo vya kike ‘Kuku Watamu’.Akizungumza na mwandishi wetu, Aunty
Lulu alisema baada ya kuandamwa na maneno juu ukaribu wake na wanaume
hao, mama yake mzazi na mpenzi wake wa sasa ambaye hakutaka kumtaja,
wamemzuia ‘kumpiga stop’ kumuona na watu hao.
“Sasa hivi ndugu zangu ndiyo wamekuwa
marafiki zangu, sitembei kabisa na kuku watamu. Siwezi kumuudhi mume
wangu mtarajiwa, mama na hata ndugu wengine, nimeamua kuachana nao,”
alisema Aunty Lulu ambaye pia ni mtangazaji ‘deiwaka’.