
Kupitia mtandao wake wa 'Instagram' msanii huyo alituma ujumbe uliosomeka hivi "Mimi ni mti wenye matunda milele siogopi kupigwa mawe"
Ujumbe huo ulionekana kuteka baadhi ya mashabiki wake huku wengine wakituma ujumbe za kumpongeza kwa kuwa na imani hiyo huku akionyesha kutoteteleka kwa jambo lolote linalomkabili ambalo linaonyesha kutaka kumdondosha kimuziki
Maneno ya ujumbe huo pia umeonekana kutumiwa katika nyimbo yake mpya inayojulikana kwa jina la 'Muziki gani' ambayo wameshirikiana na msanii Ney wa Mitego